jaridahuru

Mitandao

WC 2014: UJERUMANI YATINGA ROBO FAINALI KOMBE LA DUNIA BAADA YA KUILAZA ALGERIA KWA GOLI 2-1

Wafungaji mabao ya Ujerumani Mesut Ozil na Andre Schurrle
Mechi imekamilika . Ujerumani 2-1 Algeria .

Ujerumani sasa itachuana na Ufaransa katika robo fainali ya kombe la dunia katika uwanja wa Marakana.

Afrika sasa haina mwakilishi katika robo fainali ya kombe la dunia la mwaka wa 2014 baada ya wawakilishi wenza wa bara la Afrika katika mkondo wa pili Nigeria kushindwa mabao mawili kwa nunge na Ufaransa katika mechi iliyotangulia .

Kufutatia ushindi huu wa Ujerumani ni dhahiri sasa kuwa timu zote zilizoongoza baada ya mechi za makundi ndizo zilizofuzu kwa robo fainali ya kombe la dunia .

Ufaransa itakabiliana na Ujerumani siku ya ijumaa katika uwanja wa Maracana saa moja usiku saa za Afrika Mashariki.

Mechi itatangulia ile kati ya weneyeji Brazil na Colombia.

Jumamosi ijayo Uholanzi itakuwa na kibarua kiguimu dhidi ya Costa Rica

30:00+01 GOOOOOAL Ujerumani 2-1 Algeria Djabau

30:00 Ujerumani imefuzu kwa robo fainali
30:00 Ujerumani 2-0 Algeria Mesut Ozil
Ujerumani 1-0 Algeria 20''
17:50 Kipa wa Ujerumani Nuer anaudaka bila wasiwasi.
16:30 FREEKICK kuelekea upande wa Ujerumani na mpira unapigwa na Ibrahimi
15:30 Kipindi cha pili kimeanza kwa kasi kama kile cha kwanza lakini wanaofanya mashambulizi sasa ni Algeria .
15:00 Ikiwa mechi hii itaisha ikiwa hivi,basi inaonesha kuwa timu zote zilizoshinda makundi yao ndizo zilizoshinda mechi za mkondo wa pili.
15:00+01 Kipindi cha kwanza cha muda wa ziada kimekamilika Ujerumani 1-0 Algeria
15:00+01 Algeria wanaonekana kukubali hatima ya mechi hii
15:00 Kipindi cha kwanza kimekamilika .
13:40 Moustafa anajaribu kupenya safu ya ulinzi ya ujerumani lakini wapi
12:50 Mpira unatolewa nje na Aissa Mandi
11:00 KONA kuelekea lango la Ujerumani
02:50 André Schürrle''02 ET anaifungia Ujerumani bao lao la kwanza
02:00 GOOOOOOOAL Ujerumani 1-0 Algeria
ETRATIME
90:00+4 Mechi imekamilika Algeria 0-0 Ujerumani .Mechi hii sasa itaamuliwa katika muda wa zaida
89:00 Ujerumani inaendelea na mashambulizi lakini Algeria inahimili mikiki yao.
86:00Freekick kuelekea lango la Algeria nje tu ya eneo
Muller anakosa nafasi ya wazi
85:14
85:00 Muller anakosa fursa ya wazi
Nuer analazimika kuisadia safu yake ya ulinzi
74:30 Slimani anamjaribu Nuer kuitoka mbali lakini wapi ,Boateng anazuia duh!
71:48 Freekick baada ya Muller kuangushwa nje ya eneo
70:00 Kipa wa Ujerumani anafanya kazi ya ziada kuzuia shambulizi la Algeria.
Kipa wa Algeria anafanya kazi ya ziada
65:00
61:40 Kona kuelekea lango la Algeria ,Inapigwa na Kroos na shambulizi linazimwa .
60:00 Ujerumani 0-0 Algeria ''60
58:02 Nipe nikupe katikati ya uwanja lakini ujerumani wakionesha ukakamavu wao
Ujerumani 0-0 Algeria 62''
54:50 Shambulizi linazimwa baada ya kipa wa Algeria Rais kuutema
54:20 Kona kuelekea lango la Algeria
52:13 Andre Schurrle anapoteza nafasi nzuri mbele ya lango la Algeria .
48:41 Ujerumani wanaonekana wamechochewa kushambulia lango la Algeria
Algeria 0-0 Ujerumani 55
47:30 Kona kuelekea lango la Algeria .
46:30 Ujerumani 0-0 Algeria
46:00Kipindi cha pili kimeanza tena.
45:00+1 kipindi cha kwanza kimekamilika timu zote zikiwa hazijapata bao lolote
Kroos akishambulia Rais Mbolhi
45:10 Freekick Kuelekea lango la Ujerumani
44:50 Toni Kroos anatuma kombora lakini nje .
44:50 Algeria 0-0 Ujerumani
jaribio lingine katika lango la Algeria
41:15
37:00 Kipa wa Algeria anautema mpira mbele ya lango ,,,Nusura Muller atume kombora lakini unatoka nje na ni Goal Kick kuelekea lango la Ujerumani
36:00 Algeria wanawadhibiti Wajerumani hatua kwa hatua katika mechi hii
33:00 Leohart Frasha Lavendar matumaini ya mende kubeba kabati..,hahaha
33:00 Frank Mshana wa Tz anasema Ubinafsi ndio unatuangusha
31:10 Free kick kuelekea lango la Ujerumani nje ya eneo
30:00 Ujerumani 0-0 Algeria
Boateng na mpira !
28:30
24:45 Muller na Boateng wanashirikiana kumpokonya Soudani mpira .
23:50 Inazimwa kwa kicha na sasa imemfikia Ozil na Ujerumani wanapanga shambulizi lengine
22:30 Ujerumani inapata KONA
Slimani anapoteza nafasi nyengine alikuwa ameotea
20:45 Mechi inavyoendelea inaonesha timu zote zimetoshana nguvu
17:50 Zidane na slimani wanapoteza nafasi nyengine ya wazi mbele ya lango la Ujerumani
16:20 OFFSIDE Bao la Algeria linakataliwa kwa kuwa Slimani alikuwa keshaotea .
15:30 Ujerumani 0-0 Algeria
Mashabiki wa Algeria
12:40
10:30 Algeria Inashambulia lango laUjerumani ikibainika kuwa Slimani anamshinda kwa kasi Per Mertesacker .
08:40 Algeria wanageuza ulizni kuwa shambulizi linalomlazimu kipa wa Ujerumani kuondoka langoni ili kuzuia mashambulizi Islam Slimani
07:43 Shambulizi kuelekea upande wa Algeria .
02;50 Offside ya kwanza kuelekea upande wa Algeria .
01 Mpira unaanza uwanjani Porto Alegre
Algeria inabeba matumaini ya Afrika inapochuana na Ujerumani katik mechi ya mwisho ya mkondo wa 16 bora.
Wimbo wa taifa unachezwa
Algeria inabeba matumaini ya Afrika inapochuana na Ujerumani katik mechi ya mwisho ya mkondo wa 16 bora.
Mshindi atachuana na Ufaransa ambayo iliizima Nigeria 2-0
Mara ya mwisho Algeria iliilaza ujerumani Magharibi mabao 2-1
Algeria inakabiliana na Ujerumani.
Hii ni Mara ya kwanza kwa Algeria kuchuana na Ujerumani tangu mwaka wa 1982

Related

Worldcup 2014 3757126950261561070

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item