jaridahuru

Mitandao

MAHUSIANO: UPO WAKATI HISIA ZA MSISIMKO, KUPENDA HUPOTEA KABISA KATIKA MAHUSIANO

NI somo gumu kidogo lakini ni vizuri kulijadili maana linajenga na kustawisha uhusiano. Wengi huogopa kujifunza kuhusu hili. Ndugu zangu huu ni ugonjwa, tena hatari sana kwenye uhusiano. 

 
Kuna watu wapo kwenye uhusiano na wenzi ambao wamepoteza msisimko wa mapenzi. Yaani wanashindwa kuwa na uwezo wa kupenda. Upo uwezekano kwamba, hukumwelewa vizuri mpenzi wako mwanzoni, lakini sasa unagundua kwamba amepoteza uwezo wa kupenda.

\Suala la kushindwa au kupunguza msisimko wa kupenda ni ugonjwa! Lakini baadhi ya wahusika hufahamu tatizo hili na wengine hawafahamu. Wanaofahamu ni vigumu sana kueleza moja kwa moja kwamba wanakabiliwa na tatizo hili.

Ni vigumu sana kugundua hili mapema, lakini ukimchunguza na kuwa mkweli kwake, ni rahisi kukueleza ukweli huu uliojificha moyoni mwake.

Pengine wakati unakutana naye, alikukatalia akisema muda wa kuwa na mpenzi bado, lakini ukaendelea kumsumbua na kukukubalia, mwisho ukagundua hafurahii uhusiano wenu.

Hili huwa tatizo kubwa sana kwa walio wengi. Wakati mwingine yawezekana ukawa unafanya bidii ya kumshawishi mpenzi mpya lakini akawa katika tatizo hili.

Kila siku anakuzungusha, lakini siku moja akaamua kukueleza ukweli, kwamba anashidwa kukupenda! Huyu ni mzuri zaidi kwako, maana angalau sasa anakuwa amefahamu tatizo lake na amekupa nafasi ya kulijua, sasa wajibu wako unakuwa kumpa tiba timilifu.

IKOJE HII?
Tatizo la kutokuwa na uwezo wa kupenda, limekuwa likiwasumbua wengi sana siku hizi (hasa wanawake). Sababu kubwa zaidi ni kuwa na uhusiano wenye historia mbaya katika kipindi kilichopita!

Mwanamke aliyeachwa na wanaume watatu kwa kipindi cha miezi miwili, hawezi kuwa na uwezo wa kupenda kwa moyo zaidi kama yule ambaye ndiyo kwanza anaanza uhusiano.

Mwanamke aliyeachwa na mwanaume wake aliyedumu naye kwa miaka minne, anaweza kuwa bora zaidi katika uhusiano mpya akitaka kuokoa maisha yake ya kimapenzi kuliko yule ambaye ametoswa mara nyingi zaidi.

 
Kisaikolojia, zipo sababu nyingi zinazoelezwa kuchangia kumfanya mtu apoteze uwezo wa kupenda. Lakini sababu kubwa zaidi zilizotajwa ni hizi hapa chini;

MOSI: Anahisi havutii sana. Mara nyingi wasichana wakiachwa, huchukulia kwamba huenda hawana mvuto sana. Kwa hiyo anahisi hata kama atakupenda, akitokea mwenye mvuto zaidi yake, utamtosa kama alivyofanya aliyepita!

PILI: Huogopa ugonjwa wa moyo. Inawezekana ameshaumizwa sana huko nyuma na kila anapokuangalia anahisi kuteswa tena na hivyo anaogopa tena kupata ugonjwa wa moyo! Ana mashaka, hana amani na mapenzi tena, sababu kubwa ni historia iliyopita.

TATU: Anakuwa na mawazo kwamba, yawezekana na wewe ni sawa na mpenzi wake aliyepita. Lakini kubwa zaidi ni kwamba, mtu akiwa katika athari, akili yake yote inamwambia kwamba wote wanaweza kuwa sawa na waliopita!

Kikubwa ni kumtambua tu, baada ya hapo nitakufundisha cha kufanya. Wiki ijayo tutaangalia namna ya kumtambua kabla ya kuingia kwenye somo lenyewe na namna ya kutafuta tiba, USIKOSE!

Related

Mahusiano 2023410607583981397

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item