jaridahuru

Mitandao

FA: HATIMAE ARSENAL WAONDOA UTEJA, WATWAA KOMBE LA FA, WADAI NI MWANZO WA ARI MPYA



Baada ya kukaa muda mrefu bila kutwaa kombe lolote, klabu ya Arsenal imefanikiwa kutwaa ubingwa wa FA baada ya mechi iliyokuwa mshike mshike kwa timu hiyo.

Katika mechi hiyo iliyochezwa katika uwanja wa Wembley, timu ya Hull city iliuanzwa mchezo kwa kasi kubwa na kujipatia goli la kwanza katika dakika ya tatu ya mechezo kupitia kwa mchezaji wake James Chester. Dakika tano baadae Curtis Davies aliongezea timu yake ya Hull City bao la pili na kuwafanya mashabiki wa Arsenal kupoteza matumaini ya ubingwa.

Arsenal walipata nguvu baada ya Santi Kazola kuifungia bao la kwanza Arsenal kwa mkwaju wa adhabu katika dakika ya 17 ya mchezo.

Hata hivyo mchezo ulizidi kuwa mgumu kwa vijana hao wa wenger hadi mapumziko walikuwa nyuma kwa 2:1. Kipindi cha pili vijana wa  arsene walipata goli la kusawazisha kupitia kwa beki wao Laurent Koscielny katika dakika ya 71 ya mmchezo. Timu hizi ziliingia muda wa ziada ndipo Ramsey alipoyarudisha matumaini ya ubingwa kwa kumalizia kazi nzuri aliyoifanya Geroud na kuiandikia bao la 3 Arsenal katika dakika ya 109.

Hadi mchezo unaisha Arsenal 3:2 Hull.

Sasa Arsenal imepata kombe la kwanza baada ya miaka 9 ya ukame. Wachezji wa klabu hiyo wamesema huu ni mwanzo tu na wanatarajia kufanya mambo makubwa katika musimu ujao.

Related

Michezo 6853180394053349869

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item