jaridahuru

Mitandao

JAMII: BAAADA YA KISA CHA MTOTO WA BOKSI, KICHANGA CHAFANYIWA UNYAMA WA KUTISHA NA MAMA YAKE MZAZI


 


WAKATI tukio la kusikitisha la kifo cha ‘Mtoto wa Boksi’ likiendelea kutanda kwenye vichwa vya Watanzania, mwanamke mwingine, Fadhila Bakari, mkazi wa Keko Machungwa, Mtaa wa Championi, amefanya unyama wa kutisha kwa kutaka kumuua mwanaye muda mfupi baada ya kujifungua.


Mashuhuda wa tukio hilo, walisema kuwa Fadhila anayefanya kazi ya mama lishe, alijifungia chumbani kwake na kujifungua mtoto huyo juzi na kuanza harakati za kutaka kumuua.
Walisema kuwa walisikia sauti ya mtoto mchanga kutoka chumbani kwa mwanamke huyo, lakini walipomfuata na kumuuliza kulikoni, Fadhila ambaye alikuwa anaficha kama ni mjamzito, aliwajibu kwamba hakuna tatizo.


“Mimi ndiye nilikuwa wa kwanza kusikia sauti ya mtoto ikitoka chumbani kwa Fadhila. Ingawa mwenyewe alikuwa anaficha kama mjamzito, lakini tulihisi kama mjamzito, kwa hiyo nilidhani uchungu umempanda, niende nikamsaidie,” alisema mwanamke huyo na kuongeza.


Lakini nilipofika mlangoni, nilimuita na kumuuliza vipi, akanijibu hakuna tatizo. Jibu lake halikuniridhisha, nikamuita mpangaji mwenzangu na tukaanza kufanya utafiti. Tulimuita ndugu yake anayeishi nyumba ya jirani, alipokuja tulimueleza, lakini alipomgongea afungue alikataa.


“Ndugu yake huyo aliondoka na kwenda kumuita dada yake na walipokuja walimkuta kafungua mlango, lakini alipowaona, akataka kuufunga, lakini walimzidi nguvu na kuingia ndani,” alisema.
Jirani huyo alisema kuwa walipoingia ndani waliona michirizi ya damu kutoka mlangoni ambako wanahisi ndiko alikojifungulia, ikielekea kwenye kona ya chumba hicho ambako kulikuwa na malundo ya nguo na mifuko ya rambo.


“Dada yake alijaribu kutafuta lakini hakuona, ndipo mpangaji mwenzetu alipoingia ndani na kwenda kwenye lile rundo la nguo na alipotoa, tukamkuta mtoto amelazwa kifudifudi, tulipomgeuza, akawa anapumua kwa tabu.


“Kitu cha kwanza tulichofanya ni kumpa huduma ya kwanza, kwa kumkata kitovu, kisha tukamchukua yeye na mama yake na kumpeleka Kituo cha Polisi Kilwa Road, ambako mama huyo ameshikiliwa na mtoto anapatiwa huduma kwenye hospitali ya Polisi Barracks,” alisema.


Jirani mwingine, Andrew Kisalu, alisema kuwa kabla ya kumpeleka hospitali, walimfanyia uchunguzi mtoto huyo na kugundua amevunjwa mguu mmoja, huku akiwa na michubuko usoni kutokana na kuburuzwa na mama yake kutoka mlangoni hadi kwenye kona aliyokwenda kumficha.
“Yule mwanamke alijifungulia mlangoni, sasa inaonekana alimburuza kutoka mlangoni hadi kwenye kona kabla ya kumvunja mguu mmoja,” alisema Kisalu.


Wakizungumzia tukio hilo, wakazi wa eneo hilo walisema kuwa wameshangazwa na ujasiri wa mwanamke huyo wa kujifungua bila ya kuomba msaada kwa mtu, lakini wamesikitishwa na ukatili alioufanya wa kutaka kumuua mwanaye.


“Inaonekana alidhamiria kufanya tukio hili, ndiyo maana alikuwa anaficha kama ni mjamzito. Alitaka kujifungua kimya kimya na kumuua,” alisema.


Kituo cha Polisi Kilwa Road, kimethibitisha kutokea kwa tukio hilo, lakini wamekataa kuzungumzia lolote kwa kuwa wao si wasemaji wa Jeshi la Polisi.

Related

Jamii 6662640982803115597

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item