jaridahuru

Mitandao

SAMSUNG NOTE 7 HATARI, SIMU NYINGINE YALIPUKA TENA, SOMA HAPA





Simu ya pili ya Samsung Galaxy Note 7 iliyodaiwa kuwa salama na kampuni hiyo imeshika moto nchini Marekani,kulingana na vyombo vya habari.

Samsung ililazimika kutoa simu nyingine mpya ya simu hiyo aina ya smartphone kufuatia malalamishi ya betri zinazolipuka.
Mtu mmoja mjini Kentucky alisema kuwa alishtuka baada ya kuamka na kupata nyumba yake imejaa moshi, kulingana na vyombo vya habari nchini humo.
Hatua hiyo inajiri baada ya simu nyengine aina ya Note 7 iliokuwa imerekebishwa kushika moto ndani ya ndege ya SouthWest Airlines siku ya Jumatano.
''Simu hiyo ni miongoni mwa zile zilizorekebishwa, kwa hivyo nilidhani ziko salama,''alisema Michael Klering wa Nicholasville, Kentucky.
Aliongezea kwamba simu hiyo haikuwa imewekwa katika chaji wakati iliposhika moto katika nyumba yake siku ya Jumanne.

Related

Technolojia 5349740499656012182

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item